0

Baada ya uvumi kusambaa kuwa mchekeshaji wa kundi la Orijino Komedi  Venguamefariki na baadae kaka yake alikanusha uvumi huo, kiongozi wa kundi hilo Sekioni David amesema wamepata usumbufu mkubwa juu ya uvumi huo na wao kama kundi wameamua kuchukua hatua zaidi  ili kukomesha tabia hiyo kwa kuwa sio mara ya kwanza, wamepata ushauri kutoka TCRA ambao wamewashauri kuchukua hatua ili kuweza kujua chanzo cha uvumi huo na kuchukua hatua zaidi kwa wahusika  na muda sio mrefu mhusika atajulikana
Kuhusu Afya ya Vengu amesema ni mzima ila kutokana na ushauri wa daktari anatakiwa awe kwenye utulivu ambao unamfanya awe nje ya kundi lakini yeye bado ni mfanyakazi na anaendelea kulipwa kama kawaida.


Post a Comment

 
Top